Video za habari na matukio duniani kutoka BBCSwahili.com


BBC News Swahili

Marekani na Israel wamekuwa wakipiga mashambulio dhidi ya Iran tangu Februari 28 na kuua kiongozi wake mkuu pamoja na kulenga majeshi yake. Hakuna mmoja kati yao aliyekubali au kupinga kuhusika na shambulio lililotokea katika shule ya wasichana, baada ya Iran kutangaza kuwa watu 168 waliuawa .

Vita hivyo vimeenea zaidi baada ya Iran kuzindua makombora dhidi ya baadhi ya mataifa ya Ghuba na maeneo mengine, huku Israel ikifanya mashambulio kwenye maeneo ya Hezbollah nchini Lebanon baada ya kundi hilo la waasi kurusha makombora kuvuka mpaka.
-
-
#bbcswahili #iran #mashambulizi #marekani #israeli

1 day ago | [YT] | 151

BBC News Swahili

Aliyekuwa kiongozi wa kundi la ulanguzi wa dawa za kulevya la Jalisco cartel l‘El Mencho azikwa katika sanduku la dhahabu kwenye makaburi ya Guadalajara, nchini Mexico huku ulinzi mkali ukiimarishwa katika kipindi chote cha maziko.
-
-
www.bbc.com/swahili/articles/c5yjpkpl9kno#bbcswahi… #mexico #dawazakulevya #foryouシ

1 week ago | [YT] | 184

BBC News Swahili

Mashambulizi mbalimbali yameripotiwa katika maeneo tofauti tofauti mara baada ya shambulizi la pamoja la Marekani na Israel dhidi ya Iran na kumuua kiongozi mkuu wa Iran
-
-
#bbcswahili #iran #israeli #mashambulizi

1 week ago | [YT] | 250

BBC News Swahili

Baada ya Kifo cha Khamenei, Nani Ataongoza Iran?
Iran imetumbukia katika ukurasa mpya wa kihistoria baada ya kuuawa kwa kiongozi mkuu, Ali Khamenei, katika mashambulizi ya Marekani na Israel. Kifo chake kimeacha ombwe la uongozi katika utawala wa Jamhuri ya Kiislamu na kuanzisha mchakato mgumu wa kumtafuta mrithi wake.

Punde baada ya kuthibitishwa kwa kifo cha Khamenei, Baraza la Uongozi la Muda, lililosajiliwa huku jukumu kuu likiwa ni kusimamia serikali ya taifa, kuhakikisha utulivu wa ndani, na kuweka msingi wa mchakato wa uteuzi wa mrithi wa kudumu.

Lakini si kazi rahisi. Iran inakabiliwa na mashambulizi ya kimkakati, shinikizo la nje, na hofu kuu kuhusu nani atakayerithi nafasi ya Khamenei?
-
-
#bbcswahili #iran #masharikiyakati #marekani #Israel

1 week ago | [YT] | 141

BBC News Swahili

Huyu ndiyo Ayatollah Ali Khamenei

1 week ago | [YT] | 11

BBC News Swahili

Iran imejibu shambulizi la pamoja la Marekani na Israel kwa kuishambulia baadhi ya kambi za kijeshi za marekani ikiwemo Qatar, Bahrain na Saudi Arabia. Kusoma zaidi bofya www.bbc.com/swahili/live/cgqgldk2539t

1 week ago | [YT] | 345

BBC News Swahili

Israel imezindua kile inachokiita “shambulio la kujihami ” dhidi ya Iran. Kufahamu kwa kina kinachoendelea bofya www.bbc.com/swahili/live/cgqgldk2539t

1 week ago | [YT] | 210

BBC News Swahili

Wababe wawili wa soka la Tanzania Simba na Yanga wanatarajiwa kushuka dimbani Machi mosi huko visiwani Zanzibar kucheza mchezo wa ligi kuu Tanzania bara, Kuelekea mchezo huu Yanga ni vinara wa ligi wakiwa wamejikusanyia alama 28 pia wamewafunga Simba mara sita mfulilo
-
-
www.instagram.com/p/DVOeYUKDquB/?img_index=1
✍🏿 @loko_omi
#bbcswahili #simba #yanga #michezo #kandanda #dabi

1 week ago | [YT] | 133

BBC News Swahili

Beki wa Paris Saint-Germain, Achraf Hakimi, amesema yuko tayari kuikabili kesi yake mahakamani kufuatia tuhuma za ubakaji zinazomkabili.

2 weeks ago | [YT] | 71

BBC News Swahili

Man United chini ya Kocha Michael Carrick wamefufua matumaini ya kucheza michezo ya ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu ujao

United imeshinda michezo mitano kati ya sita iliyocheza chini ya kocha Carrick na wamefikisha alama 48, wakiwa katika nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi ya England
-
-
@loko_omi
#bbcswahili #kandanda #soka #michezo

2 weeks ago | [YT] | 121