JADI YETU DEWO OCHI

Neno JADI ni vyanzo vya kwanza vya kiutu hapa Duniani, kwa maana JA ni uwepo wa jinsia ya kwanza ya kiume kuumbwa na MUNGU hapa duniani ambaye ni Fumbakasa, na DI ni uwepo wa jinsia ya kwanza ya kike kiutu hapa duniani ambaye ni Mwasi, hivyo Jadi ni msingi wa elimu na maadili kutoka kwa mtu wa kwanza na mke wake. Kama ambavyo inavyofafanuliwa kwa usahihi kwenye zama hizi na Mcha MUNGU wa kweli ambaye ni SINGEMWAMBI TREZOLEY Mtu wa Mungu, na ndiye MWAMI LOKOKO na ROW WOMINIGE wa 786 Himu ya kuishi kwa waja, na ndio Row Wominige wa mwisho kwa muhula huu wa 71.

JADI YETU ni ukurasa unaofundisha elimu ya ukweli wa kuishi kiutu, na kweli kuhusu MUNGU na uumbaji, viumbe na mazingira kiujumla kwa ufasaha.

Kwa yeyote anayetafuta Ukweli kuhusu MUNGU na Ucha MUNGU ataupata katika ukurasa huu wa Jadi Yetu.

Mafunzo haya ya Jadi Yetu yanayotolewa na Mwami Lokoko yapo chini ya usimamizi wa Shirika la Maendeleo ya Kijamii Katika Asili na Tamaduni (SHIMKIATA).


3:03

Shared 4 months ago

1.3K views

3:42

Shared 7 months ago

950 views

5:03

Shared 8 months ago

691 views