Focus News Tanzania Tv 1, ni channel yako ya TV ya kiganjani ambapo utapata habari mbalimbali ikiwemo habari za kijamii, Siasa, Michezo na Burudani bila kusahau mahojiano katika mada mbalimbali.
Tupo Dodoma Makao Makuu ya Tanzania maeneo ya Ipagala jirani na kanisa la kwa Evance. Jiunge nasi kwa kubonyeza mandishi mekundu yaliyoandikwa Subscribe na kisha bonyeza alama ya kengere na hapo utakuwa umeungana nasi mubashara.
Akhsante kwa kuendelea kuichagua Focus News Tanzania kuwa channel yako pendwa ya TV ya kiganjani.
Focus News Tanzania Tv 1,
Mobile:.+255755834996
Whatsapp:….+255755834996
E-mail:...focusnewsroomtanzania@gmail.com
Focus News Tanzania Tv 1
LISSU ALIAMSHA “DUDE” MAHAKAMANI AOMBA SAMIA, MPANGO NA MAJALIWA KUWA MASHAHIDI KWENYE KESI YAKE YA UHAINI
Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu ameliambia jopo la majaji waliomkuta na kesi ya kujibu juu ya tuhuma za uhaini kuwa atajitetea yeye mwenyewe.
Pia Lissu amesema ataomba mashahidi wafuate ambao ataiomba mahakama iwapelekee wito wa kuitwa, amewataja shahidi wa kwanza “anaitwa Samia Suluhu Hassan,” ambaye ni Rais wa Tanzania.
Mwingine ni Philip Mpango ambaye matukio yanayolalamikiwa alikuwa mjumbe wa baraza la taifa na kama kiongozi namba mbili wa serikali.
Kassim Majaliwa wakati matokeo haya yanatokea alikuwa Waziri Mkuu na kiongozi anayesaidia serikali na kusaidia upande wa usalama wa taifa.
Lissu pia ametaja shahidi wa nne Camillus Wambura, ambaye ni mkuu wa jeshi la Polisi Tanzania.
Shahidi wa tano ni Jenerali John Mkunda, mkuu wa majeshi Tanzania.
Shahidi wa Sita ni Mkuu wa idara ya usalama wa taifa na ujasusi TISS.
Shahidi wa saba ni Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Kanali wa polisi Ramadhani Kindai.
👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/vOC28zt7DB8
6 hours ago | [YT] | 0
View 0 replies
Focus News Tanzania Tv 1
“TUTAISHAMBULIA IRAN TENA IKIBIDI” - TRUMP
Rais wa Marekani Donald Trump amesema hatasita kuishambulia tena Iran akilazimika kufanya hivyo, ili kuizuia mpango wake wa nyuklia.
Katika mahojiano na kituo cha WBBC77, Bw. Trump alisema kuwa kama si hatua alizochukua, Israel na Mashariki ya Kati zingekuwa zimeshaangamizwa kufikia sasa.
Katika mahojiano hayo, alikiri kuwa aliamuru shambulio dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran wakati nchi hiyo ilipokuwa imesalia na wiki mbili tu kabla ya kutengeneza silaha ya nyuklia.
Bw. Trump alisema kuwa licha ya kile kinachoripotiwa kwenye vyombo vya habari, Marekani ndiyo inayodhibiti Mlango-bahari wa Hormuz.
Alisisitiza tena kuwa uwezo wa Iran wa makombora na ndege zisizo na rubani (droni) umedhoofishwa sana na uchumi wake uko ukingoni mwa kuporomoka.
Bw. Trump alilitaja makubaliano ya JCPOA kuwa "janga" na kuongeza kuwa kujiondoa katika makubaliano hayo ni jambo la lazima ili kuizuia Iran kupata silaha ya nyuklia.
👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/C36z_YJTrOY
7 hours ago | [YT] | 0
View 0 replies
Focus News Tanzania Tv 1
IRAN YAONYA KUWA ITATUMIA SILAHA KALI ZAIDI KAMA KUTATOKEA VITA VIPYA.
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeonya kwamba endapo kutatokea vita vipya dhidi ya Iran, nchi hiyo itatumia silaha zilizoendelea zaidi na zenye uwezo mkubwa wa kuleta uharibifu kuliko zile zilizotumika katika mapigano yaliyopita.
Msemaji wa IRGC, Brigedia Jenerali Hossein Mohebbi, alisema Iran inaendelea kuimarisha uwezo wake wa kijeshi na kutengeneza silaha zenye usahihi mkubwa zaidi, nguvu kubwa ya mashambulizi na teknolojia ya kisasa.
👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/ky8EDoI51js
23 hours ago | [YT] | 0
View 0 replies
Focus News Tanzania Tv 1
WATU 13 WAUAWA KYIV HUKU UKRAINE IKIKABILIWA NA UHABA WA MIFUMO YA ULINZI WA ANGA.
Takriban watu 13 wameuawa na wengine 34 kujeruhiwa katika mashambulizi ya hivipunde ya Urusi yaliyolenga mji mkuu wa Ukraine, huku Kyiv ikiendelea kukabiliwa na uhaba wa makombora ya ulinzi wa anga.
Majengo ya makazi na maghala yalishambuliwa sehemu mbalimbali za jiji hilo usiku kucha, kulingana na Huduma ya Dharura ya Serikali ya Ukraine (DSNS), huku hospitali ya watoto na shule pia zikiharibiwa.
Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema kuwa ilitumia silaha za angani, nchi kavu na baharini kupiga vituo vya kijeshi na maghala, na kuongeza kuwa ndege zisizo na rubani 726 za Ukraine zilidunguliwa.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema vifo hivyo vilitokana na uhaba wa makombora ya ulinzi wa anga, ambayo Kyiv hutegemea kupewa na washirika wake wa Magharibi.
Akiandika kwenye mtandao wa Telegram, alisema "madamu Ukraine haina makombora ya kutosha ya kuzuia makombora ya balistiki, Urusi haitafikiria kwa uzito kuhusu amani".
👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/ZKFP5RDDcNU
1 day ago | [YT] | 1
View 1 reply
Focus News Tanzania Tv 1
MHADHIRI WA CHUO KIKUU DODOMA ADAIWA 'KUTAKA KUCHOMA MAJENGO YA POLISI'
Wakili wa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedeki Kitunzi Kaijage anayekabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi anasema mteja wake sasa anatuhumiwa kwamba alikuwa na nia ya kuchoma majengo ya umma pamoja na makazi ya askari Polisi katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania, ikiwemo Zanzibar.
Akizungumza Agosti 19, 2026 jijini Dodoma, baada ya kesi dhidi ya mhadhiri huyo kuahirishwa, wakili Godfrey Wasonga alisema “Si majengo ya umma tu, pia anatuhumiwa kwamba anataka kuchoma makazi ya askari Polisi Tanzania nzima ikiwepo na Zanzibar”.
Bw. Wesonga amesema tuhuma hizo zinahusisha majengo mbalimbali ya umma, ikiwemo shule, zahanati, mahakama na majengo mengine ya Serikali, huku akieleza kuwa suala hilo liko chini ya vifungu vya sheria ya kuzuia ugaidi.Wakili Wasonga amesema hatua inayofuata katika kesi hiyo ni uchunguzi wa awali, ambao unalenga kuwezesha shauri hilo kuwasilishwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kusikilizwa.
Hata hivyo, kikao cha kesi hiyo kilichopangwa kufanyika Agosti 19 kiliahirishwa kwa sababu Hakimu Mkazi anayesikiliza shauri hilo, Zabibu Mpangule, hakuwepo.
Kwa mujibu wa Wasonga, shauri hilo lilitajwa mbele ya Hakimu Kombe na sasa limepangwa kutajwa tena Agosti 27, 2026, ambapo pande zote zinatarajiwa kufahamisha mahakama hatua inayofuata.
Wakili huyo amesema siku hiyo itatoa mwelekeo wa namna shauri hilo litakavyoendelea.
👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/wdgvbNDJoq8
1 day ago | [YT] | 0
View 0 replies
Focus News Tanzania Tv 1
MWABUKUSI ACHAFUKWA, ABANWA MASWALI NA DW SAKATA LA MAWAKILI KUPIGWA MARUFUKU KUZUNGUMZA NA VYOMBO VYA HABARI MAHAKANI
Mahakama Kuu ya Tanzania imewakumbusha mawakili kutofanya mahojiano na vyombo vya habari katika viunga vya Mahakama kuhusu mashauri yanayoendelea.
Taarifa iliyotolewa na Mahakama Kuu na kusainiwa na Msajili wa Mahakama Kuu, C.M. Tengwa, Agosti 12, 2026, imesema mawakili wanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na maelekezo ya Mahakama katika mwenendo wao ndani na nje ya Mahakama.
Mahakama imesema hatua hiyo inafuatia taarifa kwamba Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kiliwataka wanachama wake kuzungumza na vyombo vya habari katika eneo la Mahakama baada ya mashauri kuahirishwa.
Hata hivyo, Mahakama Kuu imewakumbusha mawakili kutofanya mahojiano na vyombo vya habari katika viunga vya Mahakama wala kueleza mwenendo wa mashauri yanayoendelea kwa namna inayoweza kuathiri mwenendo wa mashauri hayo.
Mahakama imesema mwenendo wa mawakili, ndani na nje ya Mahakama, kuhusu mashauri yanayoendelea unapaswa kuzingatia Katiba, sheria, kanuni, taratibu na maelekezo ya Mahakama ya Tanzania.
👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/FqJMWCHRRrw
2 days ago | [YT] | 0
View 0 replies
Focus News Tanzania Tv 1
IRAN NGANGARI, YAZIDI KUIVIMBIA MAREKANI, YAWEKA MASHARTI HAYA HAPA.
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa Mlango wa Bahari wa Hormuz utaendelea kufungwa hadi Marekani itakapotimiza ahadi zake chini ya hati ya makubaliano ya maelewano ya Islamabad, ikiwemo kuondoa kizuizi na vikwazo dhidi ya mauzo ya mafuta ya Iran.
Akizungumza katika kikao cha mtandaoni cha Bunge Jumanne, Qalibaf alisema Iran inafanya kazi, kwa kuzingatia masharti na hatua zilizowekwa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Seyed Mojtaba Khamenei, kuilazimisha Marekani kuheshimu haki za taifa la Iran kupitia mchanganyiko wa juhudi za kidiplomasia na kijeshi.
“Hadi ahadi za Marekani zilizoainishwa katika hati ya makubaliano ya Islamabad zitakapotimizwa, Mlango wa Hormuz hautafunguliwa tena,” alisema.
Qalibaf alifafanua kuwa ahadi hizo zinajumuisha kuondoa kizuizi, kuachilia mali za Iran zilizogandishwa, kuondoa vikwazo dhidi ya mauzo ya mafuta, kusitisha vitisho na operesheni za kijeshi katika maeneo yote, pamoja na kutekeleza majukumu mengine yaliyoainishwa katika MoU.
👇👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/e2UNclo0tuM
3 days ago | [YT] | 1
View 0 replies
Focus News Tanzania Tv 1
KIMEUMANA, MELI 'YASHAMBULIWA' KATIKA MLANGO WA BAHARI WA HORMUZ.
Shirika la Uendeshaji Biashara ya Baharini la Uingereza linasema limepokea ripoti kwamba meli moja imelengwa na kifaa kisichojulikana, kilichorushwa kutoka angani wakati ilipokuwa ikipita kwenye Mlango-Bahari wa Hormuz.
Shirika hilo liliongeza kuwa tukio hilo lilisababisha uharibifu wa chumba cha injini na kifo cha mfanyakazi mmoja.
Kulingana na ripoti hiyo, Walinzi wa Pwani wa Oman kwa sasa wako mbioni kuwaokoa wafanyakazi wengine wa meli hiyo.
Kwa mujibu wa Shirika la Uendeshaji Biashara ya Baharini la Uingereza, hakuna uharibifu wa mazingira ulioripotiwa kutokana na tukio hilo na mamlaka zinachunguza.
👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/Rj6P0jjOhU0
3 days ago | [YT] | 0
View 0 replies
Focus News Tanzania Tv 1
IRAN YAMSHUSHUA TRUMP, YAPINGA VIKALI KAULI YAKE KUHUSU MAZUNGUMZO YA SIRI NA JESHI LA IRAN
Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amekanusha madai ya Rais wa Marekani Donald Trump kwamba Washington inafanya mazungumzo ya siri kupitia njia za nyuma (backchannel talks) na maafisa wa IRGC.
Akizungumza na Tasnim Jumatatu, Msemaji wa IRGC, Brigedia Jenerali Hossein Mohebbi, alisema hakuna mazungumzo yoyote yanayoendelea kati ya maafisa wa IRGC na Marekani.
Mohebbi alisema madai ya Trump ni “ndoto na dhana zilizotokana na kushindwa na kukata tamaa” kufuatia vita dhidi ya Iran.
Alisema IRGC ni “mkono na sauti ya nguvu ya taifa la Iran na Jamhuri ya Kiislamu”, na kwamba msimamo wake unaonyeshwa kupitia uwanja wa mapambano.
Kwa mujibu wa Mohebbi, masuala ya kidiplomasia yako chini ya taasisi nyingine za Jamhuri ya Kiislamu. Aliongeza kuwa, kwa mujibu wa taarifa zinazopatikana kwa IRGC na kauli za maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, hakuna mazungumzo yoyote na Marekani kwa sasa, hata kupitia njia za kidiplomasia.
Mohebbi alisema kutokuwepo kwa mazungumzo kunatokana na Marekani kuvunja ahadi zake na kukiuka mara kwa mara makubaliano.
👇👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/bYHv3-nPGsE
3 days ago | [YT] | 0
View 0 replies
Focus News Tanzania Tv 1
TRUMP ATISHIA KUISHAMBULIA OMAN, AMKOSOA PIA PUTIN, SUALA KUFUNGUA HORMUZ BADO NI KIZUNGUMKUTI.
Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Oman iwapo nchi hiyo itaingilia mazungumzo ya Marekani na Iran, huku akisema Washington ina mawasiliano ya moja kwa moja na maafisa wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, IRGC.
Trump alitoa kauli hiyo Jumatatu alipoulizwa na Fox News kuhusu nafasi ya Oman katika mazungumzo yanayohusu Iran na usafirishaji katika Mlango wa Hormuz.
“Iwapo Oman itaingilia, tutaishambulia vibaya sana,” Trump alisema.
Iran ilisema Jumamosi kuwa imefikia makubaliano na Oman kuhusu ramani ya njia za usafirishaji katika Mlango wa Hormuz, baada ya wiki kadhaa za mazungumzo ya kitaalamu.
👇👇👇👇👇👇👇👇
https://youtu.be/D68vGVbhyB4
3 days ago | [YT] | 0
View 0 replies
Load more