Focus News Tanzania Tv 1

Focus News Tanzania Tv 1, ni channel yako ya TV ya kiganjani ambapo utapata habari mbalimbali ikiwemo habari za kijamii, Siasa, Michezo na Burudani bila kusahau mahojiano katika mada mbalimbali.

Tupo Dodoma Makao Makuu ya Tanzania maeneo ya Ipagala jirani na kanisa la kwa Evance. Jiunge nasi kwa kubonyeza mandishi mekundu yaliyoandikwa Subscribe na kisha bonyeza alama ya kengere na hapo utakuwa umeungana nasi mubashara.

Akhsante kwa kuendelea kuichagua Focus News Tanzania kuwa channel yako pendwa ya TV ya kiganjani.

Focus News Tanzania Tv 1,
Mobile:.+255755834996
Whatsapp:….+255755834996
E-mail:...focusnewsroomtanzania@gmail.com


Focus News Tanzania Tv 1

MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI, VIFO, MAPIGANO UHARIBU WA MALI, MWENYEKITI WA WAFUGAJI AFUNGUKA.

Nchini Tanzania kumekuwa nan a matukio ya migogoro ya wakulima na wafugaji hali ambayo imepelekea chuki na uhasama miongoni mwa makundi hayo mawili katika siku za nyuma.

Ukosefu wa maji ni miongoni mwa sababu zinazoelezwa kusababisha migogoro baina ya wakulima na wafugaji na hivyo kupelekea athari kubwa katika jamii ikiwemo uhalibifu wa mali na mauaji.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/NnbUxpxhewk

10 hours ago | [YT] | 0

Focus News Tanzania Tv 1

IRAN YAZIDI KUCHOMOA BETRI, YAIKAZIA MAREKANI KUHUSU HORMUZ.

Chanzo kilicho karibu na timu ya mazungumzo ya Iran kimesema makubaliano ya mwisho yaliyofikiwa kati ya Iran na Oman kuhusu Mlango wa Hormuz hayamaanishi kwamba njia hiyo itafunguliwa mara moja.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, baada ya mazungumzo ya kina ya kiufundi na kidiplomasia yaliyofikia makubaliano mwishoni mwa Agosti, makubaliano hayo yanatarajiwa kutangazwa hivi karibuni mbele ya mawaziri wa mambo ya nje wa nchi zinazopakana na Ghuba ya Uajemi.

Chanzo hicho kimesema makubaliano hayo ni kati ya Iran na Oman pekee. Nchi nyingine zitahudhuria mkutano huo kwa ajili ya kufahamishwa kuhusu maelezo ya njia mpya na taratibu za usafirishaji, jambo ambalo linaweza kuashiria kuwa jumuiya ya kimataifa haina pingamizi na mpango huo.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Iran na Oman zimekubaliana kuhusu njia mpya za kuingia na kutoka kupitia Mlango wa Hormuz.
Njia ya kuingia katika Ghuba ya Uajemi itakuwa ndani ya maji ya eneo yanayodhibitiwa na Iran, huku sehemu ya njia ya kutoka pia ikiwa katika maji hayo. Usafiri kupitia njia hiyo utaendeshwa kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na Iran.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/SIN2WFyAk_I

1 day ago | [YT] | 0

Focus News Tanzania Tv 1

AJALI MBAYA YA MOTO DODOMA MASHUHUDA WAFUNGUKA MAZITO.

Moto mkubwa umezuka majira ya asubuhi jumamosi Septemba 12 na kuteketeza ghala la bidhaa lililokuwa katikati ya makazi ya watu katika mtaa wa Mbwanga kata ya Nkuhungu jijini Dodoma mali ya kampuni ya AM Safari lilokuwa likitumika kuhifadhi vifaa vya umeme,vyombo vya plasikiti na karakana ya mabasi ya abiria.

Uchunguzi wa awali chanzo cha moto huo kinatajwa kuwa ni itilafu ya umeme huku wananchi wakiitaka serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria wawekezaji wanaoweka maghala ya bidhaa katikati ya makazi ya wananchi hali na inapelekea madhara makubwa kwa wananchi.

Moto huo unatajwa kuteketeza ghala la bidhaa na sehemu ya nyumba iliyokuwa karibu na ghala hilo ambapo awali wakizungumza na wandishi wa habari walielezea maoni yao huku wakitaka serikali kuchukua hatua za makusudi katika udhibiti wa ujengaji maghala katika makazi ya watu.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/EEO1-VJjpJ0

1 day ago | [YT] | 0

Focus News Tanzania Tv 1

KOPA NGO’MBE LIPA MAZIWA, MPANGO UNAOENDA KUWAINUA WAFUGAJI.

Chama cha wafugaji nchini Tanzania kimesema kuwa wafugaji wa mifugo ikiwemo ngo’mbe nchni humu sasa wataondokana na umasikini kutokana na mpango wa kopa ng’ombe lipa maziwa.

Kulingana na mwenyekiti wa chama cha wafugaji nchini Tanzania, Bwana Mlida Mshota amesema kuwa mpango huo wa kopa ngo’mbe lipa maziwa utakuwa ni chachu ya maendeleo kwa wafugaji nchini Tanzania.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/c6kUsk87xXs

2 days ago | [YT] | 0

Focus News Tanzania Tv 1

KUHUSU ALIPO NCHIMBI, MBUNGE ADO SHAIBU AINYOSHEA KIDOLE SERIKALI, AIBUA MJADALA, ATOA KAULI NZITO.

Chama cha ACT Wazalendo kimetoa kauli nzito kikisema kuwa Watanzania hawawezi kukubali kuishi katika hofu ya watu kupotea huku kikihoji ni wapi alipo aliyekuwa makamu wa Rais wa Tanzania Emmanuel Nchimbi.

Kauli ya chama hicho inakuja kufuatia hivi karibuni aliyekuwa Makamu wa Rais wa nchi hiyo Balozi Emmanuel Nchini kutangaza kujiuzulu nafasi hiyo na mara baada ya hapo hajasikika tena hadharani na ajulikani alipo.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/sBz3dxFgjuo

2 days ago | [YT] | 1

Focus News Tanzania Tv 1

WATOTO 20 WAFARIKI DUNIA, SHULE MBILI ZATEKETEA KWA MOTO.

Takribani watoto 24 wa shule wamefariki katika mkanyagano walipokuwa wakijaribu kuukimbia moto ulioteketeza shule mbili katika eneo la Bukavu linalodhibitiwa na waasi, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, maafisa wa eneo hilo wamesema.

Watu wazima pia wanaripotiwa kufariki katika moto huo, na kuna hofu kwamba idadi ya vifo inaweza kuongezeka zaidi katika eneo la Kadutu lenye msongamano mkubwa wa watu.

Walionusurika wamepelekwa katika hospitali za karibu, huku picha za tukio zikionesha watoto wakiwa wamelala kwenye sakafu za hospitali huku wakiwa kwenye maumivu.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/-KYgjTKvWo0

2 days ago | [YT] | 0

Focus News Tanzania Tv 1

WATU WATANO WAUAWA, 67 WAJERUHIWA KATIKA SHAMBULIO LA URUSI DHIDI YA KITUO CHA BIASHARA, UKRAINE YASEMA

Maafisa wa Ukraine wamesema watu watano wameuawa na wengine 67 wamejeruhiwa baada ya ndege isiyo na rubani ya Urusi kulipiga jengo la kituo cha biashara katika mji wa Pavlohrad, mkoani Dnipropetrovsk.

Maduka na magari yalipigwa katika shambulio hilo la mchana, lililotokea wakati "barabara zilikuwa zimejaa watu", Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ukraine, Ivan Vyhivskyi, alisema.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Ukraine, vituo vingine viwili vya biashara katika miji ya Zaporizhzhia na Sumy pia vililengwa na mashambulizi ya anga ya Urusi mapema wiki hii.

Urusi iliripoti shambulio la ndege zisizo na rubani za Ukraine zilizorusha kutoka baharini dhidi ya mji wa kitalii wa Sochi usiku wa Jumatano, ambapo watu 28 walijeruhiwa. Pia iliripoti vifo vingine vitatu ambavyo ilivihusisha na mashambulizi ya Ukraine.

Vita kamili kati ya Urusi na Ukraine vimeendelea tangu Rais wa Urusi Vladimir Putin alipoanzisha uvamizi wa Ukraine zaidi ya miaka minne na nusu iliyopita.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/CoYrKAiSRb8

2 days ago | [YT] | 0

Focus News Tanzania Tv 1

TRUMP ATANGAZA KUMWAGA DOLA 5,000 KWA KILA MMAREKANI CHAMA CHAKE KIKISHINDA UCHAGUZI.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema atampa kila Mmarekani mtu mzima dola 5,000 iwapo chama cha Republican kitashinda mihula yote miwili ya Congress katika uchaguzi wa katikati ya muhula utakaofanyika Novemba mpango ambao unaweza kugharimu zaidi ya dola trilioni moja.

Ahadi hiyo ilitolewa katika hotuba yake kwenye mkutano wa kwanza kabisa wa chama hicho kufanyika katikati ya muhula wa urais nchini Marekani.

Trump hakutoa maelezo kuhusu mpango huo utakavyotekelezwa au utakavyofadhiliwa, akisema tu kuwa fedha hizo zitatakiwa kutumika nchini Marekani.

Makamu wa Rais JD Vance ameihusisha mipango hiyo na mapato ambayo serikali ya Marekani imekusanya kupitia ushuru wa bidhaa unaotozwa na Trump.

Mpango huo umezua utata. Wademokrasia wameuita β€œahadi tupu”, huku wengine wakihoji iwapo ahadi kama hiyo inaruhusiwa kisheria.

Huenda hii ikawa mara ya kwanza kwa rais wa Marekani kutoa ahadi ya malipo ya aina hiyo kwa Wamarekani, katika mazingira ya mwaka wa uchaguzi ambapo anawahimiza wananchi kujitokeza na kupiga kura.

Iwapo mpango huo unawezekana au la, haikuonekana kuwa jambo la msingi kwa wakati huo. Wazo hilo lilipokelewa kwa makofi na shangwe kubwa kwenye mkutano huo, huku Trump akionekana kufurahia mwitikio huo.

Kuna karibu Wamarekani watu wazima milioni 270, hivyo malipo ya dola 5,000 kwa kila mtu yangegharimu serikali ya Marekani takriban dola trilioni 1.3.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/eIOcLp1RqXA

3 days ago | [YT] | 1

Focus News Tanzania Tv 1

IRAN YASHAMBULIA KITUO CHA MAREKANI JORDAN NA KUHARIBU NDEGE ZA KIJESHI.

CBS News imeripoti, ikinukuu vyanzo vyenye ufahamu wa moja kwa moja kuhusu tukio hilo, kwamba ndege kadhaa za kijeshi za Marekani ziliharibiwa katika shambulio la makombora ya Iran dhidi ya kituo cha anga cha Mowaffaq Salti nchini Jordan mapema Jumatano asubuhi, kwa saa za huko.

Vyanzo hivyo, vilivyozungumza bila kutajwa majina kutokana na unyeti wa suala hilo, vilisema takriban ndege nane za kivita aina ya F-15 zilipata uharibifu mdogo, lakini zilirudi katika operesheni baada ya kutengenezwa.

Vyanzo hivyo pia vilisema ndege ya mashambulizi aina ya A-10 Thunderbolt, inayojulikana kama β€œWarthog”, ilipoteza moja ya mabawa yake baada ya kugongwa na kombora.

Kwa mujibu wa CBS, chanzo cha ujasusi kinachofahamu suala hilo kiliwaambia kwamba hakuna mwanajeshi wa Marekani aliyeuawa katika mashambulizi hayo.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/A_7wWFE5ur8

3 days ago | [YT] | 0

Focus News Tanzania Tv 1

IRAN YALIPIZA KISASI KWA MAREKANI, YARUSHA MAKOMBORA YA BALISTIKI, MAREKANI YAWEKA VIKWAZO MASHIRIKA YA NDEGE YA IRAN

Iran imerusha makombora ya balistiki dhidi ya kambi ya kijeshi ya Marekani karibu na Al Azraq nchini Jordan, kwa mujibu wa taarifa ya Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, IRGC, iliyonukuliwa na vyombo vya habari vya serikali.

Vyombo vya habari vya Iran pia vimechapisha video vinavyodai kuonyesha makombora ya Iran yakirushwa kuelekea Jordan. Kamandi Kuu ya Marekani, CENTCOM, haijatoa maelezo kuhusu madai hayo.

Mashambulizi hayo yanakuja baada ya CENTCOM kusema imeharibu meli tano za mafuta za Iran, Kaviz, Charminar, Horizon 1, Riesco na Derya, katika Ghuba ya Oman na karibu na Kisiwa cha Kharg.

CENTCOM imesema iliwataka wafanyakazi wa meli hizo kuondoka kabla ya kuzishambulia na kuzifanya zishindwe kufanya kazi.

Jumamosi, CENTCOM ilisema pia iliharibu meli tatu za mafuta za Iran baada ya Walinzi wa Mapinduzi kujaribu kushambulia meli ya kubeba ndege za kivita ya Marekani na meli ya kivita yenye makombora.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, amesema Iran itaendelea kupoteza meli za mafuta kila inapojaribu kushambulia meli za kivita za Marekani.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

https://youtu.be/7Ce5YausVD8

4 days ago | [YT] | 1