Deutsche Welle ni Shirika la Kimataifa la Utangazaji la Ujerumani, linaloandaa vipindi vya Televisheni, Radio na Mtandao wa Intaneti kwa ajili yako katika lugha 30 - popote ulipo ulimwenguni.

Tafadhali tusaidie kuyafanya majadiliano katika kituo hiki kuwa safi na ya kukubalika na jiepushe kutumia lugha ya kibaguzi au uchafu pamoja na matusi ya kibinafsi.

Kwa taarifa zaidi tafadhali bonyeza link ya "DW Netiquette" hapo chini.
Tunakusihi ushiriki katika utafiti wetu wa mtandaoni ili tupate maoni yako. Bonyeza kiunganishi kwa maelekezo zaidi: surveys.dw.com/c/vcemmsxp
www.dw.com/en/dws-netiquette-policy/a-5300954


DW Kiswahili

Kocha wa Misri Hossam Hassan ameeleza kuwa timu yake haikutendewa haki na kwamba maamuzi ya marefarii yalikuwa ya upande mmoja. Amedai kuwa matokeo hayo yalitokana na "dhuluma ya wazi" na hata kutangaza kuwa hatotazama tena mechi zilizosalia za Kombe la Dunia. Je, unadhani kuna upendeleo kwa baadhi ya timu au wachezaji kwenye michuano hiyo?

6 days ago | [YT] | 36

DW Kiswahili

Taswira ya Siku ya Bahari Duniani, inayoadhimishwa kila Juni 8. Kibonzo kinaangazia dhana potofu ya utupaji taka baharini na athari zake kwa maisha ya viumbe wa majini

1 month ago | [YT] | 41

DW Kiswahili

MJADALA ⚽: Timu 10 za Afrika zinashiriki kwenye Kombe la Dunia 2026!
Kuanzia DR Kongo hadi Ghana, je, nani atavuka hatua ya makundi?
Ukiangalia wapinzani wa timu za Afrika, je, kuna nafasi ya historia mpya 2026? Miaka 50 baadaye, Leopards wanarudi jukwaani. Je, wataweza kushindana na vigogo? Afrika Kusini yafungua dimba dhidi ya Mexico. Lakini makundi ni magumu—nani ataibuka mshindi? Usikose kutegea sikio mjadala huu. #DWKiswahili

1 month ago | [YT] | 32

DW Kiswahili

Je, unajua kuwa unene uliopitiliza ni miongoni mwa sababu kuu za vifo vinavyoweza kuzuilika? Tatizo hili limekuwa kimya lakini hatari, na linaendelea kuathiri watu wa rika zote. Mjadala huu unalenga kufungua macho yetu kuhusu Obesity, kwa kuelezea chanzo chake, athari zake na namna ya kuchukua hatua mapema. Lakini je unadhani unene uliopitiliza ni kosa la mtu binafsi au ni tatizo linalosababishwa na mfumo wa maisha wa leo? Tuambie maoni yako #dwkiswahili https://www.youtube.com/watch?v=cobH8...

3 months ago | [YT] | 42

DW Kiswahili

Licha ya usitishaji mapigano, shughuli za usafiri zimeripotiwa kuwa ndogo katika Mlango wa Bahari-Hormuz. Marekani imeishutumu Iran kukiuka makubaliano, Tehran nayo ikilaumu mashambulizi ya Israel Lebanon. Rais Donald Trump ameandika kwenye mtandao wake wa kijamii kwamba Iran yafanya “kazi duni sana” kuruhusu mafuta kupita. Kwingineko, Israel imemkosoa waziri wa ulinzi wa Pakistan kutokana na matamshi yake.Ukosoaji huo umejiri kabla mazungumzo yanayotarajiwa kufanyika na kati ya Marekani na Iran ambapo Pakistan ndiyo mpatanishi
Kwa mengi zaidi sikiliza matangazo yetu: https://www.youtube.com/watch?v=ddPWZ...
#DWKiswahili #Hormuz #Iran #Marekani #HabariZaUlimwengu #Nishati

3 months ago | [YT] | 17

DW Kiswahili

Wakati usitishaji dhaifu wa vita ukiendelea baada ya zaidi ya mwezi wa mashambulizi ya mabomu, Wairani wana hofu kuwa utawala uliojeruhiwa lakini unaosalia madarakani utawakandamiza zaidi wapinzani wake wa ndani. Kwa mengi zaidi kuhusu taarifa hii, basi bonyeza kiunganisho hiki www.dw.com/en/iran-war-tehran-claims-victory-but-p…

3 months ago | [YT] | 29

DW Kiswahili

Makubaliano ya Iran na Marekani kusitisha mapigano kwa wiki mbili na pia kufungua mlango wa bahari wa Hormuz ila kwa masharti, yamewaacha wachambuzi na maswali ya nani mshindi? Je, wewe mtizamo wako au tathmini yako ni gani?

3 months ago | [YT] | 81

DW Kiswahili

Trump atangaza kusitisha mapigano kwa wiki mbili nchini Iran +++ Zaidi ya watu 180 wafariki au hawajulikani waliko baada ya meli kuzama mediterrania +++ Korea Kaskazini yaendelea kurusha makombora baharini +++ Bayern Munich yaitandika Real Madrid nyumbani.+++ Kwa mengi zaidi basi bonyeza kiunganishi hiki https://www.youtube.com/watch?v=Htq9E...

3 months ago | [YT] | 23

DW Kiswahili

Maisha baada ya mauaji ya kimbari Rwanda: https://youtu.be/5FVuUrseWZQ?si=1_HJv...

3 months ago | [YT] | 4

DW Kiswahili

Watu 13 wamefariki na wengine 57 kujeruhiwa kufuatia mlipuko mkubwa uliosababishwa na moto katika kambi ya kijeshi nchini Burundi. Jeshi limesema moto huo ulizuka usiku katika ghala la kuhifadhia vifaa vya kijeshi na kusababisha milipuko kadhaa baada ya risasi na mabomu kulipuka. Msemaji wa jeshi, Gaspard Baratuza, amesema chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme, akisisitiza kuwa hakukuwa na shambulio lolote dhidi ya kambi hiyo. https://www.youtube.com/watch?v=Cgk9y...

3 months ago (edited) | [YT] | 54